SIASA

grey Mwakisole mjumbe wa kamati ya siasa CCM, akiwahutubia wananchi wa jimbo la Vwawa, Mkutano uliofanyika stendi ya Malori Vwawa mjini.




Mbozi. Idadi ya Mawaziri walioanguka katika majimbo yao imezidi kuongezeka ambapo aliyekuwa Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Godfrey Zambi (CCM) amebwagwa kwenye kinyang’anyiro cha Ubunge Jimbo la Mbozi na kijana Mwalimu Pascal Haonga (Chadema).

Zambi  ambaye alikuwa akitetea nafasi hiyo kwa kipindi cha chatu katika Jimbo hilo alijikuta akifuata nyayo za aliyekuwa ‘bosi’ wake Stephen Wasira  (CCM) aliyekuwa Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika ambaye alibwagwa na mwanadada Ester Bulaya (Chadema)  katika Jimbo la Bunda.

Mkurugenzi wa uchaguzi Jimbo la Mbozi, Edina Mwaigomole alimtangaza Haonga kwa tiketi ya Chadema kuwa Mbunge Mteule wa Jimbo hilo baada ya kupata kura 36,362 akifuatiwa na Zambi kura 34,584 na Julius Mwanitega wa chama cha Act-Wazalendo aliyeambulia kura 732.

Katika Jimbo la Vwawa Wilayani Mbozi, Mwaigomole alimtangaza mgombea wa CCM, Japhet Hasunga kuwa mbunge mteule wa jimbo hilo baada ya kupata kura 36,705 akiwa ‘amewapiku’ wapinzani wake Fanuel Mkisi (Chadema) aliyepata kura 35,400 na mgombea wa Chama Cha ACT- Wazalendo aliyeambulia kura 502.

Hata hivyo wakati wa kutangaza matokeo hayo kwa majimbo yote mawili, Zambi (CCM) hakutokea eneo la kutangazia matokeo wala hakusaini fomu ya kukubali kushindwa pamoja na mgombea wa Chadema, Mkisi katika Jimbo la Vwawa naye hakuweza kusaini fomu hiyo licha ya kuwepo kwenye  hadhara ya kusikiliza matokeo hayo.

Wakizungumza kwa nyakati washindi wa majimbo hayo, Haonga, Chadema Mbozi na Hasunga wa CCM jimbo la Vwawa walisema licha ya kuchagulia kwao kupitia vyama vyao lakini waliowachagua sio wa chama husika bali kutokana na kila mpiga kura kumuamini mtu anayeweza kuwawakilisha vyema hivyo na wao watafanya kazi bila ubaguzi wowote.

Haonga (chadema) alisema ‘Nawashukuru wananchi wa Mbozi kunipa ridhaa ya kuwa mwakilishi wao, najua nimechaguliwa kupitia Chadema lakini walionichagua ni wananchi wa Mbozi bila kujali itikadi ya Chama hivyo nawaahidi heshima walionipa sitawaangusha’.

Mgombea udiwani kata ya Ichenjezya kupitia CCM Mkola,akiomba kura kwa wananchi wa kata hiyo
Mgombea udiwani kata ya Vwawa Benard Mwazembe  kupitia CCMakimuombea kura mgombea ubunge CCM Japhet Hasunga  eneo la Ichenjezya- Kwajim
Naye Hasunga (CCM) mteule jimbo la Vwawa, alisema ‘Nashukuru sana wananchi kunipa ridhaa hii kubwa kwangu, nawaahidi nitafanya kazi na mtu yoyote bila kujali ni wa chama gani kwani aliyenipiga kura ni mwenye mapenzi na mimi. Lakini nasikitishwa na kitendo kilichofanyika juzi cha kuchomwa moto ofisi za ccm-Mbozi na Mahakama ya Mwanzo pale Mlowo kwani siasa sio vita hadi tukafika huko…’.
Viongozi mbalimbali wa Chama cha Mapinduzi wakiwa kwenye kampeni mjini Vwawa  Septemba 14  mwakja huu
Mgombea wa ubunge kupitia CCM  Japhet Hasunga jimbo la Vwawa akiwa kwenye kampeni akinadi sera zake kuwashawishi wananchi wa Ichenjezya kumchagua

Wananchi wa kata ya Ichenjezya wakimsikiliza mgombea wa ubunge CCM jimbo la Vwawa akinadi ser
Mgombea wa urais CHADEMA Edward Lowasa akiondoka Jimbo la Tunduma baada ya kuomba kura tarehe 19 Octoba 2015
Mgombea wa urais CHADEMA akiwaaga wakazi wa Tunduma baada ya kuomba kura
Mgombea urais Chadema Edward Lowasa akiwanadi wagombea Udiwani Jimbo la Tunduma tarehe 19 Octoba mwaka huu

Mgombea wa urais kupitia CHADEMA Edward Lowasa akisubiri kunadi sera zake kwa wananchi wa Tunduma tarehe 19 Octoba 2015
Wagombea  waliotangazwa leo kushinda viti vya ubunge CHADEMA jimbo la Mbozi Pascal Haonga na Japhet Hasunga CCM jimbo la Vwawa
Mgombea wa ubunge Chadema jimbo la Vwawa Fanuel Mkisi(katikati), akimpongeza mgombea wa ubunge Chadema jimbo la Mbozi kwa kushinda kiti hicho baada ya kutangazwa kwa matokeo 
Mgombea ubunge jimbo la Momba kwa tiketi ya ACT  Weston Simwelu akionekana mwenye furaha licha ya kushindwa katika kinyan'ganyilo hicho
Mgombea ubunge CCM Japhet Hasunga akilaani vikali kitendo cha uchomaji wa ofisi za CCM wilaya ya Mbozi
Baadhi ya wanachama wa CCM wakiangalia jengo lao lilivyo teketezwa kwa moto na watu wasiojulikana
Ofisi ya chama cha mapinduzi wilaya ya Mbozi yateketezwa kwa moto 
Baadhi ya mabango waliokuwa wamebeba wakazi wajimbo laVwawa wakati wa ziara ya mgombea wa urais CHADEMA  Edward Lowasa
Mgombea wa urais CHADEMA  akiwanadi madiwani wa UKAWA wa jimbo la Vwawa kwa wananchi wa jimbo hilo
Mgombea wa ubunge CHADEMA Jimbo la Vwawa Fanuel Mkisi akitoa kero za wananchi wa Vwawa kwa mgombea wa urais kupitia chama hicho Edward Lowasa tarehe 17 Octoba 2015
Mgombea wa Ubunge CHADEMA  Fanuel Mkisi  akinadi sera zake kwa wananchi wa Ilembo 
Baadhi ya ya viongozi wa CHADEMA  wakiwa kwenye kampeni eneo la Ilembo jimbo la Vwawa
Wananchi wa Ianzya kata ya Ipunga wakiapa kama watamchagua mgombea wa ubunge jimbo la Vwawa  Fanuel Mkisi kupitia CHADEMA 
Wananchi wa Ipanzya wakimsindikiza mgombea wa ubunge CHADEMA Fanuel Mkisi baada ya kumaliza kunadi sera zake katika kijiji hicho
Mgombea wa ubunge CHADEMA jimbo la Vwawa Fanuel Mkisi akinadi sera zake katika kijiji cha Ipenzya Septemba 2, mwaka huu
Mwanasheria wa CHADEMA nyanda za juu kusini akimnadi mgombea wa ubunge kwa tiketi ya chama hicho kijiji cha Ipanzya jimbo la Vwawa
Wakazi wa mji wa Tunduma wakimsikiliza mgombea wa kiti cha ubunge CHADEMA  Frank Mwakajoka eneo la stendi kuu  Tunduma
Mgombea ubunge jimbo la Tunduma akiwa kwenye kampeni eneo la Stendi Kuu mjini humo

No comments:

Post a Comment