KAMPENI ZA UCHAGUZI WA WENYEVITI WA SERIKALI
ZA MITAA CHAMA CHA CHADEMA KATA YA VWAWA
Ikiwa serikali imezindua rasmi kampeni za uchaguzi wa
viongozi wa serikali za mitaa Disemba Mosi mwaka huu Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) kimeanza rasimi kampeni
hizo za kuwanadi wagombea wao .
Katika mkutano huo Katibu Mwenezi wa chama hicho Emmanuel
Zambi amewataja wagombea wanafasi za wenyeviti kuwa ni Medelina Nyondo Mtaa wa
Haloli, Naomi Mwakasege Mtaa wa Vwawa kati, Elizabeth Kalago, Abrahamu Kalonge
Mtaa wa Mwenge , John Mkondya Vwawa Sokoni , na Ephraim Mwakateba mtaa wa Lami.
Emmanuel Zambi amewanadi wagombea hao kuwa ni wachapakazi na
wamepewa mafunzo maalumu kuhusu serikali za mitaa na jinsi ya kuongoza serikali
za mitaa kwa nia ya kuleta maendeleo pindi watakapopewa ridhaa ya kuongoza
mitaa yao.
Vilevile kwa upande wake diwani wa kata ya Vwawa Richard Kibona
amesema kuwa mji wa Vwawa unapanuka kwa kasi sana hivyo unahitaji miundo mbinu
iliyo bora inayoweza kukukidhi viwango vya mji ilikuleta maendeleo katika mji
huo kuliko hivi sasa
Kwa upande wake Dr Mgalla amesisitiza kuwa kwakipindi hiki
mabadiriko ni lazima hivyo wasifanye makosa kuto kukichagua chama hicho
kwasababu kinalengo la kuwaletea
mabadiriko ya hali ya juu kuliko ilivyo sasa.
Katibu huyo ameongeza kuwa
miundombinu duni iliopo katika mji huo inasababisha ajali kila kukicha
hivyo basi imefika kipindi cha mabadiriko wananchi kufanya uchaguzi ulio sahihi
cha kuchagua wagombea wao.
Vilevile ndugu Amanyisye amesema kuwa michango yote
inayotolewa na wananchi inatakiwa kujua idadi ya wananchi waliochangia na pesa
zilizopatikana katika uchangiaji huo ilikuwabana viongozi wenye tamaa na pesa
za walipakodi kwasababu kunabaadhi ya viongozi waliotafuna tayari pesa hizo .



