| Wakazi wa mji wa Tunduma wakimsikiliza mgombea wa kiti cha ubunge CHADEMA Frank Mwakajoka eneo la stendi kuu Tunduma |
Wednesday, 30 September 2015
Picha
Tunduma
Mwakajoka
ajifananisha na profesa
Mgombea
wa ubunge jimbo la Tunduma kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Frank Mwakajoka ametoa kali ya mwaka baada ya
kusema kuwa, mwaka huu ni mwaka wa darasa la wengi kwenda bungeni.
Mgombea huyo alisema kauli hiyo Septemba 28, mwaka
huu eneo la Stendi Kuu mjini Tunduma wakati akihutubia mamia ya wakazi wa mji
huo ambao wengi wao walionesha
kuipata vema kauli hiyo kwa kushangilia
na wachache tukishindwa kuelwa alichokimaanisha.
Mwakajoka alisema kuwa katika masuala ya kiutendaji
kwa wananchi yeye ni profesa hawezi kubabaishwa na elimu za watu.
‘’kwa kiasi kikubwa ninajua ni namna gani ninaweza
kuwaongoza wananchi wangu, na ninamna gani ninaweza kupandisha mapato ya mji wangu
hivyo basi mimi ni profesa’’ alisema Mwakajoka.
Mgombea huyo aliwaahidi wananchi wa Tunduma kuwa,
atakuwa muwakilishi bora wa wananchi katika bunge, na anatambua kuwa watu wake
wanapenda vitu bora hivyo ataifanya kazi hiyo kwa moyo wote.
Sanjari na hayo
Frank Mwakajoka alisema kuwa katika kuinua elimu atahakikisha mshahara
wake wakwanza anatangaza motisha kwa walimu wa mji huo watakao faulisha vizuri
ili kuipandisha elimu katika mji wa Tunduma.
Aliongeza kuwa ataanzisha mfuko wa elimu katika mji
wa Tunduma ambapo kuna wadau wengi wa mji huo wanaoweza kuchangia mfuko huo
ambao utasaidia katika kutatua changamoto zilipo katika sekta ya elimu mjini
tunduma.
Hata hivyo Mwakajoka aliongeza kuwa akichaguliwa
kuwa mbunge atahakikisha anamshawishi waziri wa elimu kujenga chuo cha ufundi
katika mji wa Tunduma ili wanao hitimu darasa elimu ya msingi na sekondari
waweze kupata ujuzi ili wajiajiri.
Enea Mwanja
Monday, 14 September 2015
Thursday, 3 September 2015
Wanawake wahimizwa kupigania elimu
Wanawake wahimizwa kupigania elimu
Wanawake nchini wametakiwa kuwa na umoja na
mshikamano ili kutokomeza mifumo kandamizi
inayo zorotesha maendeleo yao katika jamii hususani suala la elimu.
Wito
huo ulitolewa jana na mwanaharakati wa masuala ya kijinsia, Profesa Amina Mama
katika tamasha la jinsia 2015 lililo andaliwa na TGNP Mtandao nakufanyika
katika ofisi za TGNP Mtandao jijini Dar
es Salaam.
Profesa
Mama alisema kuwa kutokana na tafiti mbalimbali walizofanya zimeonesha kuwa
bado suala la elimu kwa mwanamke halijapewa kipao mbele hivyo wanawake
hawanbudi kufanya vuguvugu la kuipa serikali msukumo ilikuleta mabadiriko
katika mifumo yote kandamizi.
‘’Kitu
cha msingi cha kusisitiza ni suala la elimu, wanawake lazima tufanye mavuguvugu
ili kuipa msukumo serikali kuleta mabadiliko katika mifumo kandamizi’’ alisema
profesa Mama.
Hata
hivyo, Amina Mama aliwapongeza TGNP Mtandao kwa jitihada zao katika kupigania
haki za wanawake na watu walio katika makundi maalum kwa kuandaa matamasha na
warsha mbalimbali kila mwaka zinazo lenga kutoa elimu kwa jamii dhidi ya mifumo
kandamizi.
Pia
katika tafiti zake kutoka nchi mbalimbali duniani ikiwemo tafiti aliyoifanya
nchini Nigeria hivi karibuni juu ya
utekaji ya wanafunzi 300, ambapo utafiti huo ulionesha licha ya wananchi
kuandamana kutaka wanafunzi hao warudishwe lakini serikali ilionekana kuto
tilia mkazo suala hilo.
Profesa
huyo alieleza kuwa, ili kufanya mabadiliko ya kweli, wanawake wanapaswa kupaza
sauti zao kwa pamoja kuikumbusha serikali kutekeleza sera zilizowekwa
zinazotetea wanawake, watoto na watu wa makundi maalum.
Sanjari
na hayo, katika tamasha hilo linaloendelea lililoshirikisha wanaharakati kutoka
mikoa mbalimbali hapa nchini, zinatolewa warsha mbalimbali juu umuhimu wa elimu
kwa mtoto wa kike, afya ya uzazi, huduma ya maji safi na salama na ushiriki wa
mwanamke katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu
Wanaharakati
hao waliaswa kufanya mavuguvugu maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na
vijijini hata kufikia ngazi ya kitaifa
kwani mabadiliko yanayo hitajika ni yale yanayoanza kwenye mizizi
Enea Mwanja.
Tuesday, 1 September 2015
Uzinduzi wa ilani ya uchaguzi TGNP
Uzinduzi wa ilani ya uchaguzi TGNP
Dar es salaam.Wanawake nchini Tanzania wametakiwa kushiriki kikamilifu
katika mchakato mzima wa uchaguzi ili wajikwamue katika mfumo kandamizi,
uliojengeka kwa kiasi kikubwa katika jamii.
Tamko hilo lilitolewa na kaimu mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari wanawake
nchini Tanzania TAMWA Eddah Sanga wakati akizindua
ilani ya uchaguzi ya mtandao wa wanawake,
uliofanyika Septemba mosi jijini Dar es Salaam.
Sanga alisema kuwa ili wanawake
waweze kufikia malengo ya asilimia hamsini kwa hamsini ni lazima wachague
Kiongozi ambaye anaelewa matatizo yao na atakayeonesha njia sahihi ya kutatua
matatizo hayo.
“Ili wanawake tufikie malengo ya asilimia
hamsini kwa hamsini nilaziwa tuchague kiongozi ambaye anaelewa matatizo ya
wanawake.”
Hata hivyo, Eddah aliongeza kuwa wanawake ni
zaidi ya asilimia 51 ya wakazi wote wa Tanzania na wana
majukumu kubwa la kifamilia, kijamii
na Taifa kwa ujumla hivyo wana kila sababu ya kushiriki katika nafasi mbalimbali
za uongozi wa Taifa.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa TGNP Mtandao, Lillian Liundi
alisema kuwa lengo la Tamasha la mwaka
huu ni kuwasisitiza wanawake
kufanya maamuzi sahihi katika uchaguzi mkuu,2015.
Awali kabla ya kuzinduliwa kwa ilani hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya mtandao
wa jinsia nchini Tanzania(TGNP) Asen Muro alitoa historia fupi ya tamasha la
jinsia ambalo hufanyika kila baada ya miaka mitatu katika viwanja vya TGNP
Mabibo ambapo kwa mwaka huu limeanza Septemba mosi na litafikia tamati Septemba
nne.
Ilani ambayo imezinduliwa inasema kuwa Agenda ya Mwanamke, Turufu ya
ushindi 2015 ikiwa ni tamko la pamoja la mtandao wa wanawake na katiba na
uchaguzi kutoka mashirika mbalimbali na mitandao , vikundi vya kijamii zaidi ya
65 chini ya uratibu wa TGNP mtandao.
Wanaharakati hao kwa pamoja wanaamini mfumo dume kama ilivyo kwa
mifumo yote kandamizi hauwezi ukajenga mazingira ya kidemokrasia endelevu, wala
hauwezi kupunguza au kuondoa umaskini.
Enea Mwanja-Dar es salaam
Subscribe to:
Comments (Atom)