Saturday, 14 November 2015

picha

baadhi ya wadau wa taasisi zilizoalikwa kuwaelimisha wajasiliamali hao kuhusiana na taratibu mbalimbali za kibiashara kama Uhamiaji Tunduma, TRA, Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Momba , Idara ya Biashara Halmasauli ya Momba , SIDO Mkoa wa Mbeya TCCIA, SACCOS, VICOBA, TFDA na TBS

Picha

Mmoja wa wawezeshaji katika mafunzo ya ujasliamali Leons Mtana akitoa sababu ya kuwaelimisha wajasiliamali mjini Tunduma.

Wanawake wa Tunduma wafundwa

Wanawake wajasiliamali zaidi ya sabini mjini Tunduma wilayani Momba mkoa wa Songwe wamefundishwa namna ya kurasimisha biashara zao ili waweze kuzitumia fursa za kibiashara zilizoko mipakani mwa nchi kwa lengo la kuepukana na changamoto wanazokumbana katika biashara hizo.

 Mafunzo hayo yalitolewa jana na kampuni ya Tanzania Women Chamber of Commerce (TWCC) inayolenga kuwaendeleza kibiashara wanawake wajasiliamali hapa nchini. 

 Taassisi zilizoalikwa kuwaelimisha wajasiliamali hao kuhusiana na taratibu mbalimbali za kibiashara ni pamoja na Uhamiaji Tunduma, TRA, Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Momba , Idara ya Biashara Halmasauli ya Momba , SIDO Mkoa wa Mbeya TCCIA, SACCOS, VICOBA, TFDA na TBS

 Wakinamama hao walifundishwa jinsi ya kupata mitaji, kukuza na kuendeleza biashara zao kwani wanawake wengi wanaofanya biashara hizo wanashindwa kunufaika na fursa zilizopo nje na ndani ya nchi kutokana na kuwa na mitaji midogo na kukosa elimu ya ujasiliamali. 

 Mmoja wa wawezeshaji katika mafunzo hayo Leons Mtana alitoa sababu ya kuwaelimisha wajasiliamali hao kuwa ni kufanya biashara zao ziweze kutambulika kwa mamlaka husika ikiwemo kuwa na leseni ya biashara,kuwa na tini namba na kulipa mapato halali.

 Mtana aliongeza sababu nyingine kuwa kusajili majina ya kampuni kunasaidia biashara zao kuweza kuthibitishwa na Shirika la Viwango (TBS) na Mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) kwa lengo la kutangaza biashara zao na kuzifanya zikubalike katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

 Mmoja wa washiriki katika mafunzo hayo Rehema Ulivia ambaye ni mwenyekiti katika jukwaaa la wanawake kitengo cha miradi Mji wa Tunduma amewaasa wakinamama wa Tunduma kujitokeza kwa wingi zinapotokea fursa kama hizo 

 ‘’Nimejifunza faida ya kufanya biashara nje ya nchi, na nimeelewa nifuate taratibu gani kuweza kufanya biashara na nchi jirani na nawashauri wakinamama wakisikia fursa kama hizi wajitokeze kwa wingi ’’ alisema Rehema 

 Kwaupande wake Pili njebele ambaye ni mjasiliamali mjini hapo alisema kuwa kutokana na mafunzo hayo, amejifunza jinsi ya kuendesha biashara zake ndogondogo na kuziendeleza ziwekubwa ili aweze kupata mtaji wakumuwezesha kufanya biashara za kuvuka mpaka.

 Licha ya hayo, Majuma Hamza ambaye ni Afisa mtendaji wa Tanzania Women Chamber of Commerce (TWCC) amewashauri kina mama wasifanye biashara kinyemela bali watumie njia halali kwasababu wakikamatwa wanalipishwa pesa nyingi ambayo ingesaidia katika kuongeza mtaji katika biashara zao.

 Hata hivyo, Tunduma ni mji uliopo kwenye mpaka wa Tanzania na Zambia ambapo pia ni lango la kuingilia na kutokea katika nchi jirani kama Zambia na Jamuhuri ya Kidemokrasia Ya Congo, mji huo unasifika kwa biashara unazidi kukua kutokana na mzunguko wa watu ikiwa ni pamoja na wageni kutoka nchi jirani na wenyeji.

Tuesday, 27 October 2015

PICHA

Wagombea  waliotangazwa leo kushinda viti vya ubunge CHADEMA jimbo la Mbozi Pascal Haonga na Japhet Hasunga CCM jimbo la Vwawa

PICHA

Mgombea wa ubunge Chadema jimbo la Vwawa Fanuel Mkisi(katikati), akimpongeza mgombea wa ubunge Chadema jimbo la Mbozi kwa kushinda kiti hicho baada ya kutangazwa kwa matokeo 

PICHA

Baadhi ya wanachama wa CCM wakiwa katika ofisi ya halmashauri ya Momba wakipinga matokeo ubunge yaliyotangazwa na mkurugenzi wa wilaya hiyo ambapo mgombea wa CCM  Dr. Luka Siame aliyeshindwa kwa kuzidiwa na mgombea wa Chadema David Silinde

PICHA

Mgombea ubunge jimbo la Momba kwa tiketi ya ACT  Weston Simwelu akionekana mwenye furaha licha ya kushindwa katika kinyan'ganyilo hicho

PICHA

Mgombea ubunge CCM Japhet Hasunga akilaani vikali kitendo cha uchomaji wa ofisi za CCM wilaya ya Mbozi

PICHA

Baadhi ya wanachama wa CCM wakiangalia jengo lao lilivyo teketezwa kwa moto na watu wasiojulikana

PICHA

Ofisi ya chama cha mapinduzi wilaya ya Mbozi yateketezwa kwa moto 

Friday, 23 October 2015

PICHA

Mgombea wa ubunge kupitia CCM  Japhet Hasunga jimbo la Vwawa akiwa kwenye kampeni akinadi sera zake kuwashawishi wananchi wa Ichenjezya kumchagua

PICHA

Mgombea udiwani kata ya Ichenjezya kupitia CCM Mkola,akiomba kura kwa wananchi wa kata hiyo

PICHA

Mgombea udiwani kata ya Vwawa Benard Mwazembe  kupitia CCMakimuombea kura mgombea ubunge CCM Japhet Hasunga  eneo la Ichenjezya- Kwajim

PICHA

Wananchi wa kata ya Ichenjezya wakimsikiliza mgombea wa ubunge CCM jimbo la Vwawa akinadi sera zake

Monday, 19 October 2015

PICHA

Mgombea wa urais CHADEMA Edward Lowasa akiondoka Jimbo la Tunduma baada ya kuomba kura tarehe 19 Octoba 2015

PICHA

Mgombea wa urais CHADEMA akiwaaga wakazi wa Tunduma baada ya kuomba kura

PICHA

Mgombea urais Chadema Edward Lowasa akiwanadi wagombea Udiwani Jimbo la Tunduma tarehe 19 Octoba mwaka huu

PICHA

Mgombea wa urais kupitia CHADEMA Edward Lowasa akinadi sera zake kwa wananchi wa Jimbo la Tunduma tarehe 19 Octoba 2015

PICHA

Mgombea wa urais kupitia CHADEMA Edward Lowasa akisubiri kunadi sera zake kwa wananchi wa Tunduma tarehe 19 Octoba 2015

PICHA

Mgombea mwenza wa Dr John Magufuli Mama Samia Suluhu baada ya kumaliza kumnadi mgombea wa urais CCM kwa wananchi wa Mlowo tarehe 18 Octoba 2015

PICHA

Baadhi ya wasaniiwa Bongo movie wakiwa wameambatana na mgombea mwenza wa Dr John Pombe Magufuli Mama Samia Suluhu  eneo la Mlowo Jimbo la Mbozi

PICHA

Mgombea mwenza wa Dr John Magufuli Mama Samia Suluhu akimnadi mgombea wa ubunge Jimbola Mbozi Godfrey Zambi kwa wananchi wa Mlowo jimbo la Mbozi

PICHA

Mgombea mwenza Mama Samia Suluhu akimuombea kura Dr John Pombe Magufuli kwa wananchi wa Mlowo Jimbo la Mbozi 18 Octoba 2015

PICHA

Katibu mkuu wa CCM   Abdurlman Kinana akiwasili Jimbo la Tunduma kumnadi mgombea wa urais kupitia chama hicho Dr John Magufuli 16 Octoba 2015

PICHA

Green guard akiwa amesimama kikakamavu kumpokea katibu mkuu wa CCM Abdurlaman Kinana Jimbo la Tunduma

PICHA

Katibu mkuu wa CCM abdurlaman Kinana akimnadi mgombea wa uras kupitia chama hicho kwa wananchi wa Jimbo la Tunduma Octoba 16

Sunday, 18 October 2015

PICHA

Mgombea wa urais CHADEMA  akiwanadi madiwani wa UKAWA wa jimbo la Vwawa kwa wananchi wa jimbo hilo

PICHA

Mgombea wa ubunge CHADEMA Jimbo la Vwawa Fanuel Mkisi akitoa kero za wananchi wa Vwawa kwa mgombea wa urais kupitia chama hicho Edward Lowasa tarehe 17 Octoba 2015

PICHA

Mgombea wa urais kupitia chama cha CHADEMA akinadi sera zake kwa wananchi wa Jimbo la Vwawa eneo la Ilembo tarehe 17 Octoba 2015

Saturday, 17 October 2015

PICHA

Wakazi wa mji wa Vwawa wakiwa kwenye mkutano wa kampeni CHADEMA eneo la Ilembo 17, Octoba mwaka huu

PICHA

Mzee Kingunge akiwasalimia wananchi wa jimbo la Vwawa katika kampeni za Uchaguzi tarehe 17 Octoba kijiji cha Ilembo wilayani Mbozi

PICHA

Wananchi wa jimbo la Vwawa wakimsililiza mgombea wa uras kupitia CHADEMA Edward Lowasa Tarehe 17 Octoba mwaka huu

PICHA

Baadhi ya mabango waliokuwa wamebeba wakazi wajimbo laVwawa wakati wa ziara ya mgombea wa urais CHADEMA  Edward Lowasa

PICHA

Wakazi wa mji wa Vwawa wakimsikiliza mgombea wa urais kupitia CHADEMA Edward Lowasa eneo la la Ilembo

PICHA

Viongozi mbalimbali wa CHADEMA wakiwa na mke wa mgombea wa urais Mama Regina Lowasa eneo la Ilolo  Jimbo la Vwawa

PICHA

Katibu mkuu BAWACHA Taifa akimnadi mgombea wa urais Edward Lowasa kwa wananchi wa Ilolo jimbo la Vwawa

PICHA

Wananchi wa Jimbo la Vwawa wakimsikiliza mke wa mgombea wa urais Mama Regina Lowasa akimuombea kura mumewe Edward Lowasa

PICHA


Wananchi wa Jimbo la Vwawa walimsiliza Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdulrahman akimnadi mgombea wa urais CCM 

PICHA

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdulrahman Kinana akimnad ya  mgombea wa urais Dr John Magufuli kwa wananchi wa Jimbo la Vwawa eneo la Stendi ya Malori 

Habari

Kinana: Wapinzani mkipata mgombea urais mwenye sifa nitamnadi

Wananchi wa vyama vya  upinzani wameombwa kuendelee kulipa ada za vyama vyao kwani  kwasasa hawana mgombea mwenye sifa za kushika  nchi.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdulrahman Kinana alipokuwa akimnadi mgombea wa uraisi kupitia chama hicho Dr. John Mgofuli, kwa wananchi wa 
Jimbo la Vwawa wilayani Mbozi.

‘’ Kwasasa mgombea mzuri anatoka CCM  hivyo  hamnabudi kumpa kura zenu , na baadae na ninyi kwa miaka ya baadae mkipata kiongozi mzuri nitawaambia wana CCM wampe kura zote’’ Alisema Kinana.

Akiendelea kumnadi mgombea huyo  Kinana alisemakuwa Magufuli amekuwa waziri kwa miaka ishirini hajawahi kupata kashfa yoyote, wala hajawahikufukuzwa hivyo basi ni kiongozi mwadilifu na hodari.

Sambamba  na hayo, katibu mkuu huyo alitumia nafasi hiyo kuwaambia wananchi wa Vwawa kuwa Wizara ya Ujenzi aliyokuwa akiishikiria Dr. Magufuri inapokea pesa nyingi lakini hakuwahi kushawishika kupokea rushwa kwenye  wizara hiyo.

Hakuishia hapo,  Abdulrahman Kinana aliongezakuwa Mgombea wa uraisi kupitia CCM Dr Magufuli ni mtu mkweli, mtekelezaji na msimamizi mzuri na endapo watamchagua maendeleo yatapiga hatua wakishirikiana na watendaji wengine.

Licha ya hayo, Katibu Mkuu huyo alisema kuwa anawashangaa wagombea wa upinzani kwani wamekaa serikalini zaidi ya miaka arobaini nao wanathubutu kuisema serikali kama haijafanya chochote.

‘’Nawashangaa sana wagombea wa upinzani waliokaa zaidi ya miaka arobaini wanaothubutu kuisema serikali kwani wao hawakuwa viongozi basi hawana sifa za kugombea maana nao hakuna walichokifanya’’ Alisema Kinana.

Aliwataka wananchi wa Jimbo la Vwawa wapime  kuwa  mtu aliye kaa serikalini miaka mingi  anawaahidi watanzania neema kwa miaka mitano  alikuwa anafanya nini kwa miaka yote aliyokuwa ndani ya mfumo.

Hata hivyo  Abdulrahman Kinana alikiri lazima wakubali wakati wa mabadiriko umefika lakini mabadiriko hayawezi kuletwa na mtu  wa umri ulio kwenda na aliyeitwa majina yote mabaya bali mtu safi na mchapakazi.

‘’Unakuja kuleta mabadiriko umri wako wenyewe ni saa kumi na mbili jioni neema gani utakayo waletea watanzania kwa muda huo’’ Alisema Abdulrahman.


Mbali na hayo aliwakumbusha wananchi wa Jimbo la Vwawa kuwa wafanye kazi kwa bidii wasipotoshwe na kauli za wanasiasa kwani  hakuna atakaye apishwa muda huohuo na akaleta bodaboda asubuhi  maendeleo bila jasho ni kazi bure.

 Enea Mwanja

Monday, 12 October 2015

PICHA

Wananchi wa kata ya Msia wakimsikiliza mgombea wa ubunge CCM jimbo la Vwawa akinadi sera zake

PICHA

Mgombea ubunge CCM Japhet Hasunga  akinadi sera zake kata ya  Msia

PICHA

Mgombea wa Ubunge Jimbo la Vwawa Japhet Hasunga akinadi sera zake kata ya Msia kijiji cha Iyunga wilayani Mbozi

Friday, 9 October 2015

PICHA

Wanachama wa CCM wakiselebuka baada ya mgombea  Udiwani Mlki Nowa kufunga mkutano eneo la Namba One

PICHA

Mgombea wa udiwani CCM kata ya Hasanga akisalimiana na wananchi baada ya kuwahutubia wananchi wa kijiji cha Number One Jimbo la Vwawa October 9 mwaka huu

PICHA

Wanachama wa CCM na wakazi wa kijiji chja Number One wakimsikiliza mgombea wa udiwani kupitia chama hicho Malki Nzowa October 9,mwaka huu 

Wednesday, 7 October 2015

PICHA

Mgombea wa Ubunge CHADEMA  Fanuel Mkisi  akinadi sera zake kwa wananchi wa Ilembo 

PICHA

Baadhi ya ya viongozi wa CHADEMA  wakiwa kwenye kampeni eneo la Ilembo jimbo la Vwawa

PICHA

Mgombea wa ubunge CHADEMA Fanuel Mkisi  akijisajili kwenye kitabu cha wageni eneo la Ilembo jimbo la Vwawa

Saturday, 3 October 2015

Picha

Wananchi wa Ianzya kata ya Ipunga wakiapa kama watamchagua mgombea wa ubunge jimbo la Vwawa  Fanuel Mkisi kupitia CHADEMA 

Picha

Wananchi wa Ipanzya wakimsindikiza mgombea wa ubunge CHADEMA Fanuel Mkisi baada ya kumaliza kunadi sera zake katika kijiji hicho

Picha

Fanuel Mkisi akinadi sera zake kwa wananchi wa kijiji cha Ipanzya kata ya Ipunga jimbo la Vwawa