KIKAO
CHA BALAZA LA MADIWANI -MOMBA
Mkuu
huyo ambaye ana mwezi mmoja tangu aanze kufanya kazi wilaya hiyo aliyasema hayo
jana kwenye kikao cha balaza la madiwani wilaya ya Momba, ambapo alisema kuwa
viongozi wana kazi ya kuwatumikia wananchi kwani wao ndiyo walio wapa dhamana
hiyo.
Hata
hivyo aliwapongeza madiwani wa wilaya Momba nakusema kuwa hali sio mbaya ya maendeleo,
lakini kila kiongozi afanye tathimini kuwa mambo mangapi ameyafanya kwa
wananchi kwaajili ya kuwaletea maendeleo.
Licha
ya hayo bwana Mbeho alikumbusha kuwa
viongozi wahakikishe wanawahamasisha wananchi walio na umri kuanzia miaka 18
wajitokeze kwenda kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, ili
wapate haki yao ya msingi ya kupiga kura katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka
huu.
Miongoni
mwa hayo, mkuu huyo alisema kuwa viongozi wahakikishe wananchi wana fanya shughuli zao za kawaida na
kutumia fursa zilizopo ilikupata maendeleo makubwa kwa kipindi kifupi katika
hali ya utulivu na amani.
Kwa
upande wake makamu mwenyekiti wa baraza
hilo alisema kuwa ameipokea hotuba ya mkuu wa wilaya kwa mikono miwili , na wao
kama viongozi watayafanyia kazi yote kwa kushirikiana na wataalamu wao na
watafanya kazi kwa ari
Sanjari
na hayo mwenyekiti wa halimashauri wilaya ya momba Benard Sichilongwa aliwaasa
madiwani wa Wilaya hiyo kuwahimiza wananchi wao kutunza chakula ili kukabiliana na suala la
njaa linalohofiwa kujitokeza.
Vile
vile kwa upande wa mjumbe mmoja ndani ya baraza hilo aliuliza swali kuhusu
uwezekano wa kulipwa kwa wenyeviti wa vijiji, lililo jibiwa na mkurugenzi wa
wilaya hiyo Christopher Eneriko kuwa kukiwepo kwa uwezekano wa kulipwa
watalipwa na usipo kuwepo uwezekano hawata lipwa.
Hata
hivyo kwa upande wake Sapali ambaye ni diwani wakata ya kamsamba alihoji kuhusu suala la chanjo ya
kichaa cha mbwa ambapo alisema kuwa idara inachangia vipi kuhakikisha wananchi
wanaofuga mbwa wanaipata chanjo hiyo kwaajili ya mifugo yao ilikuepusha madhara
kwa watakoumwa na mbwa.
Katika
kujibu swali hilo mtaalamu wa mifugo wilaya ya Momba Deo aliahidi kufuatilia
suala hilo, sanjari na kutoa elimu kwa
wananchi na kusema kuwa suala la madawa
wameachiwa watu binafsi na sio la halmashauri hivyo basi wananchi
waelimishwe na wawewananunua madawa kawaajili ya kuchanja mifugo hata ikitokea
serikali imesaidia iwe tayari wamechukua hatua kwa usalama wao.
Na
Enea Mwanja.
No comments:
Post a Comment