KAMPENI ZA UCHAGUZI WA WENYEVITI WA
SERIKALI ZA MITAA CHAMA CHA MAPINDUZI KATA YA VWAWA
Ikiwa serikali imezindua rasmi kampeni za uchaguzi wa
viongozi wa serikali za mitaa Disemba Mosi mwaka huu Chama cha Mapinduzi (CCM)
hakikubaki nyuma nacho kimeendelea na kampeni za kuwanadi
wagombea wao zilizofanyika Tarehe 3 Disemba 2014, eneo la Ichenjezya
Kitongoji cha Mbugani .
Akizungumza katika kampeni hizo katibu Tarafa mstaafu wa
Vwawa Justina Kasunga amewanadi wagombea wa nafasi za wenyeviti wa mitaa kuwa
ni wachapakazi na wamelelewa katika maadili ya uongozi bora hivyo wananchi
wasifanye makosa kuto kuwachagua wenyeviti hao.
Aidha amesema kuwa anasikitika sana wanachama wavyama pinzani
kugeuza dhana ya vyama vingi wakidhani
kupinga na kufanya maandamano kila uchao ndio democrasia ya kweli huku wakiishia kuumiza watu wasio na hatia.
Vilevile Mama Kisunga ameonya kuwa uongozi
sio fujo, sio matusi wala
vitisho kama vyama vingine vinavyodhani
bali ni uwajibikaji na kuonesha ushirikiano na raia ilikulisukuma mbele
gurudumu la maendeleo kwa eneo atakalokuwa akilisimamia.
Licha ya hayo amesema kuwa Chama cha Mapinduzi kimewafanya
watu wawe huru, wenye amani na utulivu tangu nchi ilivyopata uhuru wake toka
kwa Wakoloni, hivyo basi amewataka wananchi kuendelea kukiamini Chama hicho kwa
kuwachagua wagombea hao.
Ameongeza kuwa mambo ya Tegeta ESCROW sio yakuyajadili kwa
sasa maana hayana manufaa kwa mwananchi mmoja mmoja bali hata fedha hizo zikitolewa
zitakuwa ni za umma hivyo si vyema wakaendelea kuumiza vichwa vyao.
Kwaupande wake mgombea wa nafasi ya mwenyekiti wa Mtaa wa
Mbugani ndugu Abdallah ameyataja mambo makuu manne atakayoyafanyia kazi pindi
akichaguliwa kuwa ni kuanzisha mfuko wa kitongoji, kusaidia vijana kupata
mikopo ya pikipiki, kusaidia wajane na wasio jiweza na kutengeneza mifereji Ya
mtaa wa Mbugani.
No comments:
Post a Comment