Uzinduzi wa ilani ya uchaguzi TGNP
Dar es salaam.Wanawake nchini Tanzania wametakiwa kushiriki kikamilifu
katika mchakato mzima wa uchaguzi ili wajikwamue katika mfumo kandamizi,
uliojengeka kwa kiasi kikubwa katika jamii.
Tamko hilo lilitolewa na kaimu mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari wanawake
nchini Tanzania TAMWA Eddah Sanga wakati akizindua
ilani ya uchaguzi ya mtandao wa wanawake,
uliofanyika Septemba mosi jijini Dar es Salaam.
Sanga alisema kuwa ili wanawake
waweze kufikia malengo ya asilimia hamsini kwa hamsini ni lazima wachague
Kiongozi ambaye anaelewa matatizo yao na atakayeonesha njia sahihi ya kutatua
matatizo hayo.
“Ili wanawake tufikie malengo ya asilimia
hamsini kwa hamsini nilaziwa tuchague kiongozi ambaye anaelewa matatizo ya
wanawake.”
Hata hivyo, Eddah aliongeza kuwa wanawake ni
zaidi ya asilimia 51 ya wakazi wote wa Tanzania na wana
majukumu kubwa la kifamilia, kijamii
na Taifa kwa ujumla hivyo wana kila sababu ya kushiriki katika nafasi mbalimbali
za uongozi wa Taifa.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa TGNP Mtandao, Lillian Liundi
alisema kuwa lengo la Tamasha la mwaka
huu ni kuwasisitiza wanawake
kufanya maamuzi sahihi katika uchaguzi mkuu,2015.
Awali kabla ya kuzinduliwa kwa ilani hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya mtandao
wa jinsia nchini Tanzania(TGNP) Asen Muro alitoa historia fupi ya tamasha la
jinsia ambalo hufanyika kila baada ya miaka mitatu katika viwanja vya TGNP
Mabibo ambapo kwa mwaka huu limeanza Septemba mosi na litafikia tamati Septemba
nne.
Ilani ambayo imezinduliwa inasema kuwa Agenda ya Mwanamke, Turufu ya
ushindi 2015 ikiwa ni tamko la pamoja la mtandao wa wanawake na katiba na
uchaguzi kutoka mashirika mbalimbali na mitandao , vikundi vya kijamii zaidi ya
65 chini ya uratibu wa TGNP mtandao.
Wanaharakati hao kwa pamoja wanaamini mfumo dume kama ilivyo kwa
mifumo yote kandamizi hauwezi ukajenga mazingira ya kidemokrasia endelevu, wala
hauwezi kupunguza au kuondoa umaskini.
Enea Mwanja-Dar es salaam
No comments:
Post a Comment