Mwakajoka
ajifananisha na profesa
Mgombea
wa ubunge jimbo la Tunduma kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Frank Mwakajoka ametoa kali ya mwaka baada ya
kusema kuwa, mwaka huu ni mwaka wa darasa la wengi kwenda bungeni.
Mgombea huyo alisema kauli hiyo Septemba 28, mwaka
huu eneo la Stendi Kuu mjini Tunduma wakati akihutubia mamia ya wakazi wa mji
huo ambao wengi wao walionesha
kuipata vema kauli hiyo kwa kushangilia
na wachache tukishindwa kuelwa alichokimaanisha.
Mwakajoka alisema kuwa katika masuala ya kiutendaji
kwa wananchi yeye ni profesa hawezi kubabaishwa na elimu za watu.
‘’kwa kiasi kikubwa ninajua ni namna gani ninaweza
kuwaongoza wananchi wangu, na ninamna gani ninaweza kupandisha mapato ya mji wangu
hivyo basi mimi ni profesa’’ alisema Mwakajoka.
Mgombea huyo aliwaahidi wananchi wa Tunduma kuwa,
atakuwa muwakilishi bora wa wananchi katika bunge, na anatambua kuwa watu wake
wanapenda vitu bora hivyo ataifanya kazi hiyo kwa moyo wote.
Sanjari na hayo
Frank Mwakajoka alisema kuwa katika kuinua elimu atahakikisha mshahara
wake wakwanza anatangaza motisha kwa walimu wa mji huo watakao faulisha vizuri
ili kuipandisha elimu katika mji wa Tunduma.
Aliongeza kuwa ataanzisha mfuko wa elimu katika mji
wa Tunduma ambapo kuna wadau wengi wa mji huo wanaoweza kuchangia mfuko huo
ambao utasaidia katika kutatua changamoto zilipo katika sekta ya elimu mjini
tunduma.
Hata hivyo Mwakajoka aliongeza kuwa akichaguliwa
kuwa mbunge atahakikisha anamshawishi waziri wa elimu kujenga chuo cha ufundi
katika mji wa Tunduma ili wanao hitimu darasa elimu ya msingi na sekondari
waweze kupata ujuzi ili wajiajiri.
Enea Mwanja
No comments:
Post a Comment