Thursday, 3 September 2015

Wanawake wahimizwa kupigania elimu

                               Wanawake wahimizwa kupigania elimu
 Wanawake nchini wametakiwa kuwa na umoja na mshikamano ili kutokomeza mifumo kandamizi  inayo zorotesha maendeleo yao katika jamii hususani suala la elimu.

Wito huo ulitolewa jana na mwanaharakati wa masuala ya kijinsia, Profesa Amina Mama katika tamasha la jinsia 2015 lililo andaliwa na TGNP Mtandao nakufanyika katika ofisi za TGNP Mtandao  jijini Dar es Salaam.

Profesa Mama alisema kuwa kutokana na tafiti mbalimbali walizofanya zimeonesha kuwa bado suala la elimu kwa mwanamke halijapewa kipao mbele hivyo wanawake hawanbudi kufanya vuguvugu la kuipa serikali msukumo ilikuleta mabadiriko katika mifumo yote kandamizi.

‘’Kitu cha msingi cha kusisitiza ni suala la elimu, wanawake lazima tufanye mavuguvugu ili kuipa msukumo serikali kuleta mabadiliko katika mifumo kandamizi’’ alisema profesa Mama.

Hata hivyo, Amina Mama aliwapongeza TGNP Mtandao kwa jitihada zao katika kupigania haki za wanawake na watu walio katika makundi maalum kwa kuandaa matamasha na warsha mbalimbali kila mwaka zinazo lenga kutoa elimu kwa jamii dhidi ya mifumo kandamizi.

Pia katika tafiti zake kutoka nchi mbalimbali duniani ikiwemo tafiti aliyoifanya nchini Nigeria  hivi karibuni juu ya utekaji ya wanafunzi 300, ambapo utafiti huo ulionesha licha ya wananchi kuandamana kutaka wanafunzi hao warudishwe lakini serikali ilionekana kuto tilia mkazo suala hilo.

Profesa huyo alieleza kuwa, ili kufanya mabadiliko ya kweli, wanawake wanapaswa kupaza sauti zao kwa pamoja kuikumbusha serikali kutekeleza sera zilizowekwa zinazotetea wanawake, watoto na watu wa makundi maalum.

Sanjari na hayo, katika tamasha hilo linaloendelea lililoshirikisha wanaharakati kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini, zinatolewa warsha mbalimbali juu umuhimu wa elimu kwa mtoto wa kike, afya ya uzazi, huduma ya maji safi na salama na ushiriki wa mwanamke katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu

Wanaharakati hao waliaswa kufanya mavuguvugu maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na vijijini  hata kufikia ngazi ya kitaifa kwani mabadiliko yanayo hitajika ni yale yanayoanza kwenye mizizi
Enea Mwanja.


No comments:

Post a Comment