Saturday, 3 October 2015

Kiama cha maandamano

Maandamano ya kukurupuka Tunduma mwisho

 Mgombea wa ubunge jimbo la Tunduma Mjini Frank Sichalwe kupitia CCM ameahidikukomesha maandamano yasiyokuwa na kibali katika mji huo ili wananchi waweze kufanya biashara zao kwa amani.

Sichalwe aliyasema hayo jana wakati akijinadi kwa wananchi wa kata ya Sogea mjini humo.

‘’Tunduma ni Mji wa kibiashara nitaulinda na kamwe siwezi kuufanya kuwa Mji wa machafuko, sitakuwa chanzo cha kufunga biashara zenu hata kwa saa moja kwasababu ya maandamano’’.Alisema Sichalwe.

Mgombea huyo alifafanua kuwa maandamano ni haki ya msingi kwa kila mtanzania, lakini maandamano yana utaratibu wake lazima yapate kibali kutoka polisi, ili wananchi waweze kufikisha ujumbe kwa serikali yao kwa amani.

Frank aliwasihi  wananchi wa Tunduma kuwa, wasitumiwe kama daraja la uvunjifu wa amani kwani viongozi wa juu wa vyama vya siasa  ni marafiki na  muda mwingi wanakuwa pamoja iweje wanatunduma wawekeane uhasama kwaajili ya vyama.

 Enea Mwanja


No comments:

Post a Comment